Listing 5000+ Islamic books in more than 30 languages. Read online or download in PDF.
1. Mfalme wa majini
Abu Saad ‘Abdallah Bin Ahmad alisema, ‘Safari moja, binti yangu Fatimah alitoweka kutoka katika paa la nyumba.basi nikapatwa na wasiwasi na kwenda katika ukumbi wenye baraka wa Sultani-ul-Auliya, Sheikh Ghauše-A'zam رَحْمَةُ اللهِ تَعَالٰی عَلَيْه na nikamlalamikia. yeye. رَحْمَةُ اللهِ تَعَالٰی عَلَيْه, Akasema ‘Nenda mji wa Karkh na kakae nyikani wakati wa usiku na utengeneze upweke uzio wa kiroho (yaani mduara) wewe na nafsi yako tu. usome ﴿بِسۡـمِ اللّٰه﴾ na utafakari juu yangu. Katika nyakati za usiku, misafara mingi ya majini itapita karibu na wewe. Nyuso zao zitakuwa za ajabu na za kutisha. Wakati wa daku, mfalme wa majini atakuja kwako na atakuuliza nini shida yako,basi utamwambia, ‘Sheikh 'Abd-ul-Qadir Jilani رَحْمَةُ اللهِ تَعَالٰی عَلَيْه amenituma mimi kutoka Baghdad na kanipa ujumbe unitafutie binti yangu aliepotea.
Kwa maana hiyo, mimi nikatoka Karkh na nikayafuata maelekezo ya Ghaus-e-A'zam رَحْمَةُ اللهِ تَعَالٰی عَلَيْه. Ndani ya ukimya wa usiku ule, majini wenye kutisha wakawa wanapita kwenye uzio wangu. Nyuso zao zilikuwa ni za kutisha kiasi kwamba sikuweza kuvumilia kuziangalia. Wakati wa daku, mfalme wa majini alikuja akiwa amepanda farasi pamoja na majini wengine. Alikuwa amebakia nje ya uzio na kuniuliza, ni shida yako. Mimi nikasema kwamba Ghaus-e-A'zam رَحْمَةُ اللهِ تَعَالٰی عَلَيْه alikuwa amenituma kwako. Kusikia vile tu, akashuka farasi na kukaa chini. Majini wengine wakaifanya hivyo hivyo na kukaa chini ardhi nje ya uzio. Mimi nikamsimulia kisa ya binti yangu aliye
BOOK TOPIC
BOOK TOPIC